mardi 17 septembre 2013

AUSTRALIA : LILL"P nyota inayozidi kungaa'ara Mjini BRISBANE/Australia...




LILL"P
NIYINTUNZE Privato a.k.a LILL"P ni msanii wa kizazi kipya ambae azidi kunga'ara nchini Australia kwa upande wa tasnia ya mziki . Kijana huyo mwenye umri wa miaka 20 alizaliwa kusini mwa nchi ya Burundi ,Tarafani Nyabigina , Komine Nyanza-Lac , Mkoani makamba sehemu wasanii wanaotamba nchini Burundi walipozaliwa nikizungumzia kama Uncle Crazy, Mkombozi , Fizzo japo alizaliwa Tarafani Bwiza /Bujumbura , alikuwiya Mkoani Makamba ,  ... LILL"P kwasasa anaishi Mjini BRISBANE/AUSTRALIA na familia yake .
Anatamba pande zile na pini 2 * DESPISE , GIVE ME A CHANCE TONIGHT inayofagiliwa sana pande zile kwa mashahiri na beat inavyokwenda sambamba na mistari *,pini hizo zilitengenezwa na producer Mrundi anaejulikana kwa jina la Fabio na studio yake ikijitangaza kwa jina la ' IFABIO Production " kijana huyo alituhamisha kuwa yuko mbioni kuachiya pini yake ya kwanza atakayo imba akitumiya lugha ya kiswahili na kirundi lugha yake ya taifa kwani izo mbili za kwanza alizi imba kwenye lugha ya kingereza, na nyimbo hiyo ameipa jina * I'm Free *,itatengenezwa ANGLES STUDIOS niya wazungu . Alitwambia :" Niko studio kwa sasa,nilishafanya booking ,kinachosalia nimimi kuingiza sauti najuwa haitokuwa rahisi ila ntajitaidi kadri niwezavyo , na washabiki zangu nina imani kuwa watakubali ."
http://thumbp4-ir2.thumb.mail.yahoo.com/tn?sid=960696922&mid=ALgk5C4AAAckUjWZAAAAAFfxT%2FA&midoffset=2_0_0_1_1111912&partid=5&f=1725&fid=Inbox&w=614&h=472
LILL"P

Aliongeza kutufahamisha :" Mimi nilizaliwa Burundi ila nilipatoka nikiwa badi kinda sana ,nakuwa na shahuku zakuja kuona nilipotupa kitiofu ,na hivi karibuni napanga kuja jutembea ,kisha niko na plan yakutumika na Wasanii wanyumbani kwani nia ninayo nikukuza na kudumisha upendo na kufanya mziki wa Burundi na warundi wanao imbiaya hapa tuwe kitu kimoja ."

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire