mercredi 3 juillet 2013

Clip Video 2 za CHUMA CHA CHUMA zitakufikieni hivi karibuni...


Msanii wa mitindo ya kipekee Chuma cha Chuma, Sharobaro wa Burundi aliongea na safu yetu hii akawa ametuwekea wazi kuwa :" Ifikapo Jumaa-pili hii Kampuni ya Alfa System watanichukuwa picha za clip ya nyimbo * Kizunguzungu* , lakufahamu lingine nikuwa video ya nyimbo niliomshirikisha Fizzo *Kibaju baju* iko tayari."Niko kimya kwa upande kwani nimebanwa na shughuli nzima yakufundisha kingereza , ila akipenda Mungu baada ya mwezi mtukufu wa Ramadhani ntaachia pini kadhaa zitakazo kuja kunitambulisha zaidi. Kwa upande wa maisha ya kawaida alitufahamisha kuwa :" Niko kwenye heka heka yakufunga ndoa na mtoto wa kiarabu atakae onekana kwenye 1 kati ya clip."

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire