samedi 23 février 2013

Primus league: -Muramvya: Match ya Royal na Vital'o fc imehomba baada ya mlima kuporomoka uwanjani na watu 6 kuponea kupoteza maisha...



Primus League daraja la kwanza nchini burundi leo hii ilikuwa imeingia kwenye wiki yake ya 11, Jijini Muramvya timu ya Royal fc imeipokea Vital'o fc bingwa tetezi mwaka jana na vile vile ikiwa ni timu mija wapo inayowakilisha Burundi kwenye mashindano ya Club bingwa barani Africa . Match ya leo ilikuwa imezungumziwa sana kwenye vituo vya radio flani flani nchini kama match ya wapinzani wawili ambao kila mmoja aitaji kuchukuwa namba ya mungine kwani Vital'o fc yao ilikuwa tayari inamchezo umoja wazaidi,yaani yao match ya leo ilikuwa ya mwisho huku Royal fc ilikuwa bado ina match nyingine baada ya wki 2 . Hali alisi iliotokea ni kuwa walipokuwa tayari wameshacheza dakika 31 za mchezo huo kimanga manga kilianguka uwanjani na kidogo kama Sio mungu kupita kati kingelisababisha mafa,kwa ripoti tunayo hadi mdaa huu ni kuwa watu walio anguka nakufunikwa na kimanga manga hicho wote walirekebishia hospitalini ( Hospital kuu ya KIGANDA) nawakawa wamepata nafuu,na hadi mdaa huu wameziwiliwa hospitalini. Match hio ilikuwa imetandwa na uchawi wa hali ya juu kwa hali tulio ishighudia na pengine alisema mpenzi mmoja wa timu ya Vital'o fc ambae tunamuhufadhi jina kuwa :" Royal walikuwa wamekubali kutowa watu kafara ili wafunge Vital'o fc" . Shutma hizo hatuna nazo uhakika pengine ikawa tu ni usemi wamshabiki . Ifahamike ya kuwa timu hio ambayo iko inawania tiketi yakushiriki ngazi ya 16 ya mashindano ya Club bingwa barani africa ikiwa kwenye mapambano na timu ya majeshi ya Rwanda ilikuwa imeshindikizwa na halaiki ya watu kwenye pambano hilo ambalo lilikuwa na upinzani wa hali ya juu. Duru kutoka chama cha mpira nchini kimeamuwa match hio kuchezwa tarehe 6/March/2013 kwenye uwanja wa Mwanamfalme Louis Rwagasore  kwakusubiri kurekebishwa uwanja wa Kiganda,Jijini Muramvya .

Matokeo mengine: Atletico Olympic 0 - 1 Flambeau de l'Est.
                             Espoir Mutimbuzi 0 - 1 Inter Star.

Ratiba ya kesho Jumaa-pili : LLB Ac. - Academie Tchite.

N.B : Kutokana na gisi tulikuwa kwenye orodha ya wachezaji wa Royal,hatukupata gisi yakuchukuwa picha za tokio hilo,tunawaomba samahani.

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire