mardi 31 décembre 2013

Kampeni ya " You'll Love Changes Vol. 1 " inatangazwa pande za Tanzania...




Pichani : Vincent Kigosi a.k.a Ray na Mr H.
Jumaa-pili tarehe 29/December/2013 ndipo Mkurugenzi mkuu wa kampuni ya IKOH MULTISERVICE IKORICIZA HARUNA a.k.a Mr H alisafiri kwa ndege aina ya AIR TANZANIA kuelekeya Mjini Dar Es Salaam kutangaza kampuni yake ya IKOH  pande zile kuhusikana na Kampeni (Project) yake ya " You'll Love Changes Vol.1 " . Fahamu ya kuwa Kampeni hiyo , shaba kubwa nikuyaleta mabadiliko nchini Burundi kwa upande wa entertainement kwa ujumla .Tanzania ambao wao wamepiga hatuwa kwenye kanda hii wamepewa shavu na MR H ili waungane naye kwa ufanisi wa Kampeni hiyo , kumbuka ya kuwa alishafanya ziara kadhaa nakukutana  na Watu wengi tena muhimu kwa upande wa muziki, filamu... Miezi ya nyuma alikuwa nchini Kenya  kukutana na KIDUM , bila shaka kwa moyo mkunjufu alimkubaliya kuwa ataungana naye . Tulipozungumza naye ,alitufahamisha kuwa :" Niko Tanzania kwa muda kutangaza mpango mzima wa kampeni ya You'll Love Change's , nimeshaonana na baadhi yao kama VINCENT KIGOSI , JB , AUNT EZEKIEL, na bado ningali na gahunda yakukutana nawengi wengi . Wengi wao wamekubaliana nami kuhusikana nakutowa mchango wao ambao utakuwa ni muhimu kwa kuendeleza Entertainement nchini Burundi ." Aliendeleya nakutufahamisha :" Nitazifanya interview nyingi kwenye baadhi ya Vituo vya redio na TV nchini Tanzania kwa niya yakuitangaza Kampuni ya IKOH ." Fahamu ya kuwa alifkiya kwenye Hotel yakifahari Mjini pale inayojulikana kwa jina la ' WANYAMA HOTEL Ltd ' .

Tizama baadhi ya picha akiwa Mjini dar es salaam :

Akiwa anachangiya na Mhariri Mkuu wa www.ikoh.biz
Mhariri wa Ikoh Ally Bilali  akiwa na Vincent Kigosi.
Mr H akiwa Wanyama Hotel Ltd
Mr H akiwa kwenye Uwanja wa ndege Mjini Bujumbura.

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire