lundi 28 octobre 2013

Breaking news: BABA MZAZI WA WEMA SEPETU,BALOZI ISAAC SEPETU AFARIKI DUNIA

Habari zilizotufikia hivi punde mtandao huu wa www.sufianimafoto, zinasema kuwa, Baba Mzazi wa msanii wa Filam nchini na Miss Tanzania wa mwaka 2006, Wema Sepetu, Balozi Issac Abraham Sepetu, amefariki Dunia asubuhi ya jana tarehe 27/10/2013 katika Hospitali ya TMJ Mikocheni jijini Dar es Salaam, alikokuwa amelazwa.
Aidha imeelezwa kuwa, Balozi Sepetu alikuwa amelazwa katika hospital ya TMJ akitibiwa ugonjwa wa Kisukari na kiharusi uliokuwa ukimsumbua.
Hadi umauti unamkuta,Balozi Isaac Sepetu alikuwa ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Uwekezaji wa Vitega Uchumi Zanzibar.
Mtandao huu unaungana na waombolezaji wote wa Msiba huu na Mwenyezi Mungu, Aiweke Roho ya Marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu, Mahala Pema Peponi.

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire