dimanche 25 août 2013

Confederation Cup ( 1/2 final ) : Lydia Ludic Burundi academic 1 - 0 Atlhetico Olympic 0...

Jana Jumaa mosi tarehe 24/8/2013 kwenye uwanja wa Mwanamfalme Louis Rwagasore ndipo palipochezeka mchuano wa kwanza kwenye ngazi ya  Nusu fainali. Jana kwenye uwanja huo watani wa jadi wawili Lydia Ludic burundi academic ilimenyana na Atlhetico Olympic kwakuwania tiketi yakuicheza fainali ya kwanza ya kombe lilochukuwa na fasi ya kombe la Raisi miaka 3 ya nyuma na kubatizwa jina la Kombe la Shirikisho ( Coupe de la Confederation ) . Anakae tunzwa tunzo hilo moja kwa moja anakuwa balozi wa Burundi kwenye ngazi ya kombe la shirikisho barani africa kama inavyo iwakilisha Burundi LLB miaka 3 iliopita . Mchuano wa jana ulikuwa ni wavuta nikuvute kwani timu zote 2 kila moja iliwasili uwanjani kuja kuonyesha kipi unacho cha ziada kwa nyingine timu . Wachezaji wa Athletico ka Ciza Hussein na Nahimana Claude almaarufu kama Papa Claude wanao semekana kuwa watajiunga na Mukura ya Rwanda kwa ushirikiano na wenzao walionyesha kandanda safi na kosa kosa zikawa nyingi kwenye lango la LLB lililo lindwa na mkongwe Nyabenda Athanase alias Tchimba alie onekana kuwa mpole sana na mtulivu golini . Kosa kosa hizo za Athletico zilikuja kuwasababishia kufungwa bao na NDARUSANZE Claude baada ya shuti kali iliopigwa kama mshale na NDUWARUGIRA Christophe alias Lucio ,mpira huo maskini ya mungu Nduwimana Saidi alias Tamaa ulimshinda ukawa umemtoka na ndipo Claude ali iwezeshea timu yake kupata bao hilo muhimu sana ilikuwa ni kwenye dakika ya 44 ,dakika 1 kabla ya muda maalumu  kumalizika wa kipindi cha kwanza . Walipotoka mapumzikoni  hapakuwepo mabadiliko yeyote ngambo zote mbili kwa mmoja kuona lango la mwenzie. LLB ina sura nzuri yakuchukuwa tunzo hilo baada yakulitetea taifa  vyakuridhisha kwenye michuano hio yakibara miaka 3 ya nyuma na hadi walipofika kwenye mchuano wa mwisho ungeliweza kutuma wafike hadi kwenye duru ya makundi mwaka huu baada yakuchapwa kitunga cha mabao na timu tajiri ya Mali STADE MALIEN (5-0 , 1-0 ) . Matumaini ni yote kwa upande wa Mkufunzi TUHABONYE Michel ambae anakiri kwa udi na uvumba lazima wanyakuwa tunzo hilo . Nani watakae pambana kwenye fainali ? Timu itajulikana kwenye mchuano wa leo kati ya Academie Tchite na As Tanganyika , timu ya daraja la pili ambayo ilifika mwaka  huu kwenye ngazi hio...Wait and see.

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire