jeudi 10 octobre 2013

MKOMBOZ :" Patachimbika Musee Vivant tarehe 13/10/2013"

" Baada ya kimya kirefu , nilikuwa natunga nitoke vipi ", hii ni kauli aliyo ongeya Mkomboz baada ya kuwa alizungumzwa mengi kipindi cha nyuma . Aliongeza nakusema :" Burundi iko na wasanii kibao wanao ujuzi wa hali ya juu kwa upande wa tasnia ya muziki, na ndiyo kwa maana hiyo niliketi chini nakutafakari nifanye kipi kitakacho kuja kuwa kinyume na yaliyo andaliwa na wasanii wenza kipindi cha nyuma , ndipo nikaja kugunduwa fikra nzuri nikuchangiya jukwaa na wakubwa zangu kimziki , ndiyo kwa maana nitakuwa na wengi hapo tarehe 13/10/2013 ,itakuwa vile vile fursa yakuwakumbuka wamarehemu waliyo saidiya Burundi kufika pahali ilipo kwasasa kwa upande wamaendeleo ." Fahamu ya kuwa Msanii huyo ambae alijijengeya jina muda mfupi kwa mitindo yake ykukemeya mambo flani flani yanayojiri nchini yasiyokwenda sawa na heshma ya raia . Mkomboz anaweza kuwa ni msanii anaeshikiliya rikodi ya kufanya show kwa uzinduzi wa nyimbo moja nakushangiliwa na raia wengi . Bada ya *URUDUBI * , tarehe 13/10/213 itakuwa ni uzunduzi wa * Umubanyi wanje * , nyimbo iliyogubikwa na ujumbe mkali uliyokwenda shule . tizama hapo juu kwenye bango mpangiliyo mzima .

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire