mardi 3 septembre 2013

World news : Mwanamke Wa Miaka 64 Avunja Rekodi Kwa Kuogelea Kutoka Cuba Mpaka Florida, Atumia Masaa 52, Amefanikiwa Baada ya Kujaribu Mara 35, Fahamu Zaidi hapa


Mwogeleaji mwenye umri wa miaka 64 kutoka Marekani, Diana Nyad ameweka rekodi mpya ya dunia katika kuogelea baada ya kufanikiwa kuogelea kutoka Havanna Cuba mpaka huko Florida Marekani.Ikiwa hii ni mara ya 35 mfululizo kufanya jaribio kama hili na kwa jumla ya hesabu, ameweza kukaa ndani ya bahari kwa masaa 52, dakika 54, na sekunde 18.6, na aliweza kutoka mwenyewe mpaka beach kabla ya kuishiwa nguvu kabisa. Safari ya mwanamama huyu imekuwa na umbali wa jumla ya maili 110 sawa na kilometa 180.
 
Safari zote ambazo mwanamama huyu amekuwa akijaribu kuvuka bahari amekuwa akipata changamoto kama vile kushambuliwa na samaki wakali wa baharini na mambo mengi ya kufanana na hayo lakini hakukata tamaa kujaribu tena na tena na safari hii amefanikiwa bila kutumia vifaa vya kujikinga.


Mwanamama huyu amesema kuwa amejifunza kuwa katika safari ka kufuatilia kutimiza ndoto zako, usikate tamaa hata siku moja, na hakuna swala la kizuizi cha umri katika kufuatilia ndoto zako.





Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire