lundi 11 mars 2013

Lolilo ametupwa korokoroni...( Lolilo yatawe mu mvuto...)

Msanii NIYONZIMA Salum Nassor a.k.a Lolilo amekamatwa leo asubuhi saa ine na askari polisi mtaani Nyakabiga anapoishi. Habari tulizozipata tulipofika sehemu alipofungwa tulijaribu ku uliza kisa na maana chakumfunga,tulijulishwa kuwa ni habari ndefu,na wakawa wametwambia kuwa ntajulishwa kesho . Baada ya hapo kama mdaa wa saa sita mchana nikaendelea na uchunguzi nakuitaji kujuwa hasa kisa na maana nikawa nimpata mtu wa karibu sana na Lolilo ambae aliniomba nisimtaji akawa amenibainishia haya yafwatayo :" Lolilo toka saa ine asubuhi (10h) anafungwa kwenye kituo cha Polisi  Tarafani Nyakabiga kutokana na shutma za binti anaejulikana kwa jina la Claudine anae dai kuwa ni mpenzi wa Lolilo, anasema kuwa Lolilo alivunja vitu vyake vya ndani akimaanisha (TV,Radio,Viti,Kabati...) alivunja vitu hivyo baada ya kumkuta binti huo ambae adaiwa kuwa alikuwa mpenzi wake akiwa na mwanaume mungine , hakufuraishwa nakuona hali hio na ndipo kufanya tokio hilo lakuvunja vitu hivyo  ,baadae Mwanadada huo ambae alikuwa alimwambia kuwa anauja uzito wake (ana mimba yake)  Lolilo akawa ameikana , akawa ameona hakuna njia nyingine isipokuwa kutafuta atakae ikuza nakuigharamia . Kwa upande mungine Lolilo yeye alipo ulizwa alikana kuwa hawezi kulipa chochote kwani yeye ndie alimgharamia vyote vilivyokuwa ndani , na ndico chanzo chakusalia korokoroni ." Alimaliza nakutwambia kuwa uchunguzi bado hadi mdaa huu unaendelea,uyo ndio ukweli alikuwa anaufahamu kuhusikana na tokio hilo... Shutma hizo ni za kweli? Ni kweli Lolilo njo alimgharamia vitu vyote hivyo alivyo vivunja? Na je msichana huo anauja uzito wake ? hayo ni maswali ambayo bado tunajiuliza,jawabu itakapo patikana nina imani kuwa tutawawekeya yote bayana . Itaendelea...

 N.B : Hatukupata na fasi yakupiga picha kwani tulimkuta anafungwa , yani hatukupewa na fasi yakumuona.

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire