mercredi 27 novembre 2013

VINCENT KIGOSI :" Sina hofu kuwa IKOH MULTISERVICE italeta mabadiliko kwenye nchi ya PETER NKURUNZIZA." ."

Saa saba usiku jana :Ray, Hansy , Juma na Emile aliyewaleta buja wakila pozi la mwisho kwenye Uwanja wa ndege.
Wasanii wa tasnia ya filamu kutoka nchini Tanzania wameitembeleya ofisi ya kampuni kubwa yenye malengo makubwa yakubadili mambo yaliyokuwa yanasuwa suwa kwa upande wa tasnia ya music na filamu kiujumla entertainment . Kwa muujibu wa habari tulizoshughudia nakufwatiliya kwa ukaribu ni kua Vincent Kigosi , Oprah , Miriam , Juma CHIKOKA na Hansy Chuchu walikuwa ziarani Burundi kwenye mualiko wa Kampuni inayo ongozwa na Emile ili waje kutowa mchango kwenye uzinduzi wa filamu waliyokuwa wameigiza . Walivyokuwa wanasubiriya Wasanii hao siyo waliyo yakuta kwani wao walisubiriya kuwa watapokelewa kwenye Hotel ya kifahari zinazo jizatiti vyumba vizuri na swiming pool na kadhalika wakajikuta wamekaribishwa kwenye Hotel za chochoroni na wao papo hapo kukata katu katu kufkiya kwenye Hotel Hiyo . Baada ya ya mdaa wa saa 4 wakiwa wamewasili bujumbura ilipigwa sim ya rambi rambi kutokeya DUBAI na Mmiliki wa kampuni ya IKOH MULTISERVICE nakuomba wanayo isimamiya Burundi wawapokeye wasanii hao na wawafikishe kwenye Hotel yeyote ili bila kujali gharama .

Roca Golf Hotel : Anzo Mafia Mnyama akila pozi na RAY
Pichani : HANSY , OPRAH na MIRIAM
Ndipo ABDALLAH SHOKOLOKO, msimamizi akawa ametumiya mdaa huo vizuri nakuwazungu usha kwenye Hotel zote kubwa kubwa Mjini kama Source du Nil , Novotel ya zamani , Star Hotel , Sun Safari Hotel ,wao wakawa wamependekeza ROCA GOLF HOTEL na ikawa bila pengamizi yeyote na usiku huo huo wa tarehe 22/11/2013 IKOH ikawa imelipiya vyumba 2 ( RAY na HANSY ambao niwapenzi kama alivyodhihirisha mwenyewe RAY, room namba 408) na Juma CHIKOKA , room namba 407 .
Hii ni resiti (Reçu) ya malipo .
IKOH kiukweli ilidhihirisha kuwa inataka kuyaleta mabadiliko kwa upande wa Entertainment nchini baada yakulipiya gharama ya milioni tatu,laki mbili na elfu ishirini na na moja, miasaba na hamsini (3.221.750 sarafu za burundi ) , sawa na dola 2068.87 sarafu za marekani , ikiwa imetokeya kama ghafla kwani Wasanii hao hawakuwa na mpango ao mazungumzo yoyote na Kampuni ya IKOH . Ilitokeya baada ya Jamaa waliyowaleta Burundi kushindwa kukidhi maitajiyo yawo. IKOH daima kuleta marekebisho mbali mbali kwenye nyanja tofauti nchini Burundi .

Mahali pote walikuwa hawaachani wapenzi hao...
Pichani :Irene Uwoya , Miriam na Mr Abdallah...
Haikuishiya hapo kwani iliwa alika Wasanii hao kwenye Ofisi zake Mjini kati na walipata fursa yakuweka bayana fikra na kudhihirisha shukrani zao kwa Kampuni hiyo baada yakuchangiya chakula cha saa sita wakiwa pamoja na Watangazaji AMIDOU HASSAN , Dj RAPHAN , AISHA AMURI na Jopo (Crew ) nzima ya IKOH . Picha walipofika kutembeleya IKOH MULTISERVICE :

Wasanii hao walizungumza yafwatayo :

* VINCENT KIGOSI : IKOH MULTISERVICE kwa Burundi ni Studio kubwa sana , nimeshanga kuikuta . Nawapa sifa wamiliki wa studio . Nilipokutana naye kwa mara ya kwanza Mjini Dubai mwezi wa 6 mwaka jana nilipokuwa ziarani kule alinidokezeya Kampeni yake ya ' You'll Love changes ', nikamuakikishiya kuwa ntajiunga na Project hiyo bila pengamizi kwani niligunduwa kuwa MR H ni kijana anaejituma sana na nimzalendo , anapenda nchi yake sana vinginevyo angefunguwa studio kama hiyi nchi nyingine angelipata pesa nyingi sana , sina hofu kuwa IKOH inakuja kuyaleta mabadiliko kwa upande wa Entertainment kwenye nchi ya PETER NKURUNZIZA ." Aliomba kwakumaliziya interview yake fupi Crew ya IKOH inayoendelesha kazi Burundi  :"Vijana pigeni kazi kwani ndiyo siri ya mafaanikiyo , kazi maafanikiyo kwanza baadae ."

* IRENE UWOYA a.k.a OPRAH : IKOH MULTISERVICE ni kiboko, yaani nooma ,mimi ni mara kadha kuitembeleya Burundi ila nilikuwa sitegemeyi kuwa panaweza kuwa watu wenye roho yakupenda nchi yao kama MR H , anapaniya kweli kuyaleta mabadiliko nchini ,nampongeza sana na wale wote wanae shirikiana naye kwakuweka sawa ndoto zake . Nilikuwa sifahamu chochote kuhusikana na Kampeni ya 'You'll Love Changes' , ila ninafkiri akinidokeza ntakuwa na mchango muhimu wakutowa ki fikra na kiufundi zaidi. "

Fahamu ya kuwa ziara yao ilimalizika hapo jana , na walisafiri saa saba usiku kuelekeya Mjini Dar Es Salaam .

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire