dimanche 28 juillet 2013

Orodha ya Wachezaji 11 wa Burundi wanaoweza kuanza zidi ya mchuano wa marudio na Sudan ya Kaskazini...

Blog yenu kulinganisha mchuano tulio uona wa awali Jijini Bujumbura na gisi wanavyojipanga wachezaji wa timu ya Sudan , hapana shaka kuwa Coach Mkuu Nassim Loftty atapanga wachezaji ifwatavyo :

Golini : Arakaza Mc Arthur
Winga wa kulia (2) : Rashid Léon
Winga wa kushoto (3) : Hakizimana Hassan l'Homme (C)
Walinzi wa nyuma (4 na 5) : Issa Hakizimana na Kaze Gilbert Demunga
Kiungo wa katikati : Duhayindavyi Gael , Nduwarugira Christophe Lucio , Ndikumana Yussuf Lule
Washambuliaji : Nahimana Papa Claude, Célestin habonimana na Tambwe Amissi.

Ifahamike ya kuwa mshindi kati ya timu hizo mbili atakuwa ameipata fursa yakuingia moja kwa moja kwenye mashindano ya CHAN yatakayochezwa nchini South africa mwezi January/2014. Kipenge cha mchuano huo kimepangwa kupulizwa rasmi saa tatu usiku (21h) saa za Bujumbura,sawa na saa ine saa za Kharthoum.

Tunawatakia ushindi...

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire