lundi 1 avril 2013

RDC: Wachezaji 3 wa DC Motema Pembe waliofariki tarehe 28/March/2013 watazikwa tarehe 3/April/2013 jijini Kinshasa...


Kandanda ya Jamuhuri yakidemkrasia ya Congo ipo msibani . Wachezaji 3 wa Timu ya Daring Club Motema Pembe , GoalKeeper Guelor Dibulana , Hugues Muyenge na Mozart Mwanza , walifariki dunia kwa ajali yabarabarani usiku wa tarehe 28/march/2013 Jijini Kinshasa bada yakugongana na gari ya wanajeshi . Kwenye ajali hio aliekuwa anaendesha gari waliokuwa emo Mbindi na wengine wawili waliumia vibaya na hivi wako hospitalini . Baada ya ajali hio Viongozi wa imu hio waliamuwa kulaza miwili ya wachezaji hao kwenye hospital Saint Joseph ya Limete . Jana timu hio ilikuwa ipambane na Vita Club ila uongozi wa soka nchini pale waliamuwa kuahirisha pambano hilo kwenye tarehe hadi mdaa huu haijafahamishwa . Kwa upande wa Coach mkuu Epoma Fanfan wa timu hio anasema kuwa :" Wametuachia pengu likubwa mno kwani ni wachezaji ambao nilikuwa tayari nimesha waweka kwenye mpango wakuwa wanaanza kwenye orodha ya 11 wa mwanzo ,ila tuliwapenda sisi Mungu akawapenda zaidi ." Kwa upande wakiongozi (President) wa daring Club Motema Pembe Antoine Musanganya anasema :" Mazishi yamepangwa kufanyika tarehe 3/April/2013 Jijini Kinshasa . Kuna uwezekano wa timu kusafiri kuelekea Nchini Burundi kuchuwana na Lydia Ludic Burundi Academic pambano ya duru ya marudiano ya ngazi ya 16 (1/16 final) ." Ifahamike ya kuwa bao pekee lililofungwa kwenye pambano ya awali lilifungwa na hayati Mwanza kwenye dakika ya 89 . Timu ya DC Motema Pembe iliundwa mwaka 1936 .

Wachezaji waliotamba miaka ya nyuma kwenye timu hio ni pamoja na :

Kibiasi Vignal, Ebumba Piola alias Tarzan, Ntela Henri, Paul Bonga Bonga « Gonano »,Holden Roberto, Max Mayunga Rick Coppens, Jules Balondo, Julien Kialunda, Androkwa, Ngelebeya Englebert, Odjudjua, Miranda, Mpase Carré, Elifa, Léopold Kisuaka, Likimba, Muwawa Pélé, Gaby Nsay, Tuntu martin, Gaston Nganga Dafirma, Kalambay Roger Sukisa, Damena Damar, Mondonga Mombito, Ossango, Kiala Petit Puscas alias Decoulo, Essamba, Makiadi Castello, Dondo, Raph Montonga, Djuma, Makelele Soucous, Domingos, Bosete Vicky, Miolo Rigoudi, Kidumu Raoul, Muana Kassongo, Kabamba Serpent de Rail, Freddy Mulongo, Itele, Babayila Sofia, Kalonji Amalphi , Makindu Anita, Bessy Hebreux, Marc Malamba, Body, Mongongu, Makombo Alidor, Major Kamulembe, Mampuya Lepère, Nsingi Jacques, Totimo, Mayenda Mayens, Tunda Samy (gardien), Tebakula (Tebens). Mubiayi Juif, Lewula (gardien), Kilasu, Ebengo Souplesse, Pélé Lembe, Manu Kakoko, Osei Koffi, Maetens, Akuda, Mukalayi, Katanga Mullër, Lessendjina, Bokomo Jungle, Mandiki, Fifi Nzuzi, Bukaka Paul, Sambi, Mbungu Tex, Mbungu Dereck, Pembele Ngunza, Misato, Bokote Gabon, Mboyo, Kapesa, Mudindu Océan, Ngandu Eddy Morgan, Kongi I et Kongi II, Kiyika, Fila, Longange, Kabasu, Matuka, Mobezo, Mizele, Mateta, Ndjibu, Ilonga, Banana, Bwana Ngalula, Makiadi Luyindula, Basawula Payne, Mahungu Lutovoka, Mapuata Richard, Kuba, Danga (petit poisson), Pupa, Kinuani, Mboni,.Kufua, Mwape, Masombo, Kalonda (Turbo), Kakoma, Mboyo, Lokondo (Serpent), Mukendi Kamikaze, Inkina, Sisi Shokoto, Lembi I, Mayala, Pala, Makengo, Bunene, Mwanza Mirage, Bobutaka, Moke Adede, Nsuka Mero, Mbinga, Diavovoka, Mpoy, Emeka Mamale, Masudi, Ndinga Mbote, Ikina, Ibuka, Kavuanda, Ngambio, Nginamau Le Fou, Mpasi Silawuka, Abiti, Nkongolo (gardien), Mwanza Mirage, Alima Monga, Merikani Godis et Merikani Zembla, Bulayima, Ngombo, Mandiangu, Mbiyavanga Maestro, Matudidi Shora, Ngongo, Kidoda, Bunene, Bondali Swing, Muanimi Mbembe, Ngunza, Kazanga, Kirongozi, Lunkulu, Okitakatshi, Samy Mata, Kialanda Myra, Fuala Buteni, Mukanza Ferros, Lukisu Techn, Dimbuana Kadet, Ngubi,...

Tunawapa pole timu na familia za wachezaji hao...

Kenya : KIDUM Live Accoustic

Tarehe 18/May/2013 Mwanamuziki kutokea burundi atatimuwa vumbi akitumia alaa (instruments) na kundi lake la Boda Boda band.

FABRICE BIRORI :" Video 8 zangu mpia zitakufikieni hivi karibuni..."

Msanii wa miondoko ya hip hop toka nchini Burundi BIRORI FABRICE amelonga na BB akawa ametuwekea wazi kuwa yuko kwenye harakati zakumalizia mlolongo wa picha zakuona (video) za nyimbo zake 8 na vile vile kuachia leo hii pini yake mpia itakayosimama na jina la "Abantu nkamwe" aliomshirikisha WILLY SIRABAHENDA mmoja kati ya wasanii waliokuwa wanaunda kundi la Etoile du Centre . Alitwambia :" Niko natumika na Golden Star pamoja nae KOOK KAY videos nane , hivi karibuni zitakuwa zimemalizika ,ni na imani kuwa Washabiki wangu watapa uhondo tosha kwani tumetumia ufundi wa hali ya juu ,tumejitaidi kadri na uwezo wetu kuonyesha hali halisi ya vituko , ushauri wa maneno tuliokuwa tunaimba kwenye nyimbo hizi 8 ambazo ni pamoja na 1.Reka nkwibarize 2.Ubwoko bwimamba 3.Abantu nkammwe 4.Africa 5.Ntibakiri isoko 6. Mama 7. Tamaa 8. itangazo ..." Ifahamike ya kwamba FABRICE BIRORI yumo katika kundi la Bold Boys pamoja nae Chris B NDINDI

BOTCHOUM PRO, PRODUCER ASIE CHAKAA



Utakuwa ni ukosefu wa fadhila iwapo utauzungumzia muziki wa kizazi kipya nchini Burundi bila kutaja jina la Producer Botchoum Pro, aliejizolea sifa tele katika kuandaa na kutengeneza muzizi wa wasanii wengi wa kizazi kipya walioibuka miaka ya 90 na kuanza kuonyesha makeke kwenye tasnia hii ya Muziki ambayo ilianza kitambo tu, na Wasanii waliobeba majina makubwa kama vile akina hayati Chanjo Amisi, Christophe Matata, Afrika Nova Bahaga Prosper na wengine ambao waliwavutia sana wapenzi wa muziki wa Burundi katika zama hizo.


Kwa jina halisi ni Kwizera Freddy Khaled maharufu kama Botchoum alianza kucheza muziki kama Disc Joker ama DJ na baadae kuwa muandalizi wa Muziki kwenye Studio ya kwanza aliko anzia Felix Music iliokuwa chini ya mkono wa Felix Music aliekuwa DJ katika Club Archipel mwaka 2003.

Akiwa Feliz Music aliweza kutengeneza nyimbo za wasanii wengi chipukizi walioibukia tasnia ya muziki wa kizazi ambao leo wamejijengea majina na wengine waliaomuwa kuondoka kwenye game la muziki.


Akilonga na Ikoh Biz Botchum amesema kwamba katika kipindi hiki tayari amepata mafaanikio makubwa lakini pia amekuwa akikutana na misukosuko ambayo ni kawaida katika kila nyanja ya maisha kukumbana na mauzauza.

Botchoum amesema kwamba ndoto yake kubwa ni kujiimarisha zaidi katika kazi yake, ili siku moja aweze kufanya kazi na wasanii wakubwa Dunia.

Kwa sasa Botchoum amesema anatulia kwenye Studio ya Kampuni ya Ikoh Multiservice kuhakikisha anainuwa wasanii wengi ambao wanania ya dhati ya kusonga mbele kwenye kwenye tasnia hii ya Muziki ambayo amesema inahitaji bidii ya kutosha na nguvu za ziada ili kuendelea kuwepo kwenye muziki.

Source : Ikoh