dimanche 14 avril 2013

Confederation Cup : LYDIA LUDIC BURUNDI ACADEMIC 2-0 DCMP.(Inaendelea kwenye ngazi ya 1/8 final)

Yapata miaka karibu 20 , nchi ya Burundi ilikuwa haijapata fursa yakuivuka ngazi ya ngazi ya 16 (1/16 final) . Lydia Ludic imepata fursa hio baada tu ya leo kujishindia mchuano wa marudiano kwa bao 2-0 , bao zilizofungwa na NDARUSANZE Claude (15') na DUHAYINDAVYI Gael (55') , kwenye kipindi cha kwanza LLB Academic ilipata na fasi yakupachika bao la pili baada ya mchezaji Idi Saidi Juma kuchezewa rafu na hivo basi refa hakusita kuwapa penalti iliokuja kuokolewa na kipa wa DCMP Moussa Sylla kwenye dakika ya 47' . Mchuano huo ulizibitiwa kipindi kikubwa na LLB japo kosa kosa za huku na kule hazikukosa . Bao la pili lilifungwa na Gael kwenye dakika ya 55' , dakika 10 walipotoka kwenye mapumziko . LLB Academic  imekuja kuikomboa Burundi baada ya miaka zaidi ya 20 kutofuwa dafu yakutambuka ngazi ya 16 (1/16 final) yaani toka mwaka 1991 . LLB itachuwana na ASEC MIMOSA kwenye ngazi ya 8 (1/8 final) , mchuano wa duru ya awali umepangwa kuchezwa Jijini Abidjan (Ivory Coast) . Hongera sana vijana wa Coach MICHEL ...

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire