mercredi 24 avril 2013

Wabalozi wa Burundi kwenye mashindano ya SICA/Benin mwaka huu ni ALFRED na BERNARD...

Mashindano ya SICA yanayofanyika nchini Benin mwaka huu , Burundi itawakilishwa na NYANDWI Alfred na NDOREYICIMPA  Bernard , vijana wawili wanao ondoka na mitindo ya ki utamaduni ndio watakuwa Wabalozi wa Burundi kwenye mashindano hayo . Ikumbukwe ya kuwa mashindano hayo yanayofanyika kila baada ya mwaka umoja na Burundi tayari kushiriki miaka kadhaa na bahati nzuri imeshajaliwa kupata nafasi yakushinda : ( 2009 Steven Sogo na 2012 Emelance Emy ) . Vijana hao wawili tayari wameshajaliwa kuzuru nchi 8 kabla yakwenda kupanda Benin , na nchi hizo ni pamoja na : China mara 2 , Japon , Ethiopia , Cameroun , Kenya , Rwanda , Senagal na Congo-Brazzaville. Safari imepangwa mwezi wa November ila hadi mdaa huu hawajatambuwa watasafiri aje kwani uwezo bado haujapatikana na ndio kwa maana hio Kiongozi wa Baraza la Wanamuziki nchini , vile vile yeye akiwa kama Kiongozi wa SICA kwenye kanda ya maziwa makuu Mh Bruno SIMBAVIMBERE alias MEMBER anaomba wale wote ambao wanaipenda nchi yao wajitoleye ili mpango mzima wa safari ya Vijana hao ukamilike .

* Kumbukumbu :

-2009 : Steven Sogo IRAMBONA ( * Il est beau mon pays * , ilipata tunzo ya nyimbo bora )
-2010 : Albert KULU
-2011 : HARERIMANA Shazzy Cool 
-2012 : Emelance Emy NIWIZERE ( * Yambogorera * , ilipata tunzo ya clip video bora )

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire